Jinsi YouTube wanavyo lipa ???

Image result for how to get youtube money
Je ulishawahi kujiuliza ni jinsi gani YouTube Huingiza Pesa??
          YouTube huingiza Pesa kwa njia ya kuonyesha Matanga Kwenye Chanel yako ni kama vile Television Ya Habari au kituo cha Radio kinavyo ingiza Pesa Ndefu kupitia  MATANGAZO. Basi Youtube nayo hufanya hivyo hivyo. Ni kwa njia gani basi hayo Matangazo huingiza Pesa.
  1. Kupitia Views
  2. Kupitia Subscriber
  3. Kupitia likes 
  4. ku click Matangazo (lakini hii usifanye wewe kwani wakigundua wata suspend chanel yako)
  5. Kutazama Matangazo kwa Muda Mrefu(Unaweza ukafanya lakini usi click Tangazo)

Je wale wenye views nyingi kama Diamond Platnumz ndio hupata fedha nyingi zaidi? Ni views ngapi unazohitaji ile kuingiza fedha kwenye YouTube? Hili ni swali la kawaida ambalo watu huuliza na jibu lake litategemea na nani umemuuliza.
Unaweza kuwa umesikia kuwa utaingiza dola moja kwa kila views 1,000 au $1,000 kwa views milioni moja. Wengine husema ni $5 kwa views 1000.
Mtandao wa videopower.org unadai kuwa tunauliza swali lisilo sahihi na kwamba tunatakiwa kuuliza ‘ni engagement gani inayohitajika ili kuingiza fedha kwenye Youtube?
Mtandao huo unasema huingizi fedha kwa kuzingatia kiasi cha views unachopata. Unatengeneza fedha kwa kuzingatia engagement ya watu kwenye tangazo.
Hapa engagement inamaanisha ni mtu kubofya na kuangalia tangazo kwa zaidi ya sekunde 30. Matangazo ya YouTube yanawezesha kwenye mfumo wa Adwords. Makampuni huchagua kuweka matangazo kwa njia mbili kuu; Cost Per Click (CPC) au Cost Per View (CPV).
Cost Per Click (CPC)
CPC ni pale kampuni inayotangaza inalipa fedha kwa kuzingatia clicks. Kwahiyo kama keyword fulani ikiwa na CPC ya $3 na mtu akaclick tangazo hilo, itaichaji kampuni hiyo $3. Maneno haya ya matangazo hutokea chini ya screen wakati unatazama video na huweza pia kutokea kama banner ya square upande wa kulia wa channel yako.
Cost Per View (CPV)
CPV ni pale kampuni inayotangaza inalipa fedha kwa kulingana na views. View kwa kampuni inayotangaza (advertiser) inamaanisha kuwa mtu anaangalia tangazo kwa walau sekunde 30 au nusu ya tangazo.
Mtu huyo anaweza kuclick tangazo hilo hata mara 50 lakini bado kampuni inayotangaza isitozwe kwasababu hailipi kwa click, wanalipa kwa view.
Kampuni inayotangaza hulipa tu pale mtu anapoclick au kuangalia tangazo kwa sekunde 30. Hii ndio maana huwezi kugeuza views za channel yako kuwa fedha. Kama video yako ikiangaliwa mara milioni 10 lakini hakuna mtu aliyeangalia au kuclick tangazo, huwezi kuingiza fedha yoyote.

Comments

Popular posts from this blog

Jinsi ya ku promote YouTube Chanel Yako watu waka ifahamu kwa wingi ?

Zijue Njia za Kienyeji katika Kuongeza YouTube Views na Subscriber ??

JINSI YA KUPIGA PESA NDEFU KUPITIA BLOG BUREE